Friday, April 12, 2013

NI WIKI YA MAJONZI MAKUBWA KWA KIFO CHA JOSEPH LEOPORD RWEYEMAM

ilikuwa jumamosi tarehe 6 april 2013 nilipopokea simu iliyo haribu siku yangu.ilikuwa ni simu ya kunitaarifu kuhusiana na ajali iliyotekea mkoani shinyanga maeneo ya kahama na ikinitaka kufuatilia na kujua wahusika katika ajali hiyo wana hali gani, kutokana na umbali niliokuwapo kufika eneo la tukio ilinilazimu kutafuta jamaa yangu aliekuwa kahama na kumuomba afuatilie habari hii, kwakweli habari nilizokuja letewa toka kwa rafiki yangu huyo hazikuwa na matumaini baada ya kunambia mtu mmoja aliyekuwa ajali hiyo amefariki na wengine wamejeruhiwa vibaya. huo ndo ulikuwa mwisho wa uhai wa ndugu yetu na rafiki yetu JOSEPH RWEYEMAM. nakumbuka mwaka 2008 kwa furaha kubwa nilipost hapa harusi yake na leo kwa huzuni kubwa na post habari ya kifo chake. tulikupenda joseph lakini Mungu alikupenda zaidi. R.I.P Joseph Rweyemam