Monday, June 22, 2009

PIGO KUBWA KATIKA MUZIKI WA TAARABU


Mwimbaji wa siku nyingi wa muziki wa Taarab aliyewahi kutamba na kundi la muungano lililokuwa likiongozwa na Mchezea nyoka maarufu Norbert Chenga Nasma Khamis "Kidogo" amefariki dunia leo kwenye Hospitali ya Temeke alikokuwa amelazwa kutokana na kuugua Maralia
Baba mdogo wa Marehemu ambaye amejitambulisha kwa jina la Mzee Kaniki akizungumza na vyombo vya habari nyumbani kwake Kinondoni Sharif Shamba ambako ndiko msiba uliko amesema Marehemu alikuwa na matatizo ya shinikizo la damu tatizo lililokuwa likimsumbua mara nyingi, hata hivyo siku za hivi karibuni alishikwa na maralia na kupelekwa katika Hospitali ya Temeke ambako alilazwa na kukaa hapo kwa siku nne mpaka mauti yalipompata usiku wa kuamkia leo
Nasma Khamins atakumbukwa kwa nyimbo zake nyingi nzuri zilizokuwa zikipendwa na mashabiki wengi wa muziki kama vile "Naona mambo iko huku" wimbo uliovuma sana wakati huo akiwa na kundi la muungano kundi hilo likiwa hasimu mkubwa wa kundi lingine la la muziki wa Taarab TOT, ambapo mwimbaji mshindani wa Nasma alikuwa alikuwa Khadija Kopa Mungu ailiaze mahali pema peponi Roho ya Marehemu Nasma Khamis Kidogo Amin

1 comment:

Yasinta Ngonyani said...

Kaka mbona umepotea upo salama?