Wednesday, October 31, 2007

NILIKUWA KWENYE MAOMBOLEZO


ingawa sikuwashirikisha lakini sivibaya kama mkijuwa kwamba nilikuwa kwenye maombolezo ya rafiki yangu mpendwa na dada yangu kipenzi prisca Nkanyila aliye fariki kwa matatizo ya figo. ni kifo ambacho kimeniuma sana ukizingatia alikuwa bado mschana mdogo ambaye taifa lilikuwa likisubiria mchango wake.vilevile ni pigo kubwa kwa familia yake ukizingatia baba yake mzazi mzee nkanyila alifariki miezi miwili iliyo pita. alikuwa mwaka wa pili katika chuo kikuu cha ushirika moshi. pamoja na kugharimu figo yamdogo wake na kupelekwa matibauni nchini India bado mungu alimuhitaji zaidi. niliahidi kuiweka picha ya prisca nkanyila hapa sasa sikufanikiwa kuipata aliyo piga mwenyewe.kwa kumtambua prisca ni aliye vaa blauz ya bluu au wa3 toka kulia.

10 comments:

Egidio Ndabagoye said...

Mkuu nilipata haabri hizi kwa masikitoko makubwa sana.

Namkumbuka sana Prisca.Alikuwa mpole,mtulivu asiekuwa na makuu.Nakumbuka siku 2 kabla ya kuja huku nilikuwa nae.
Nakumbuka aliweza kunipa moyo ushauri kwa baadhi ya mambo fulani.

Kweli tutakukumbuka Prisca.RIP

chemshabongo said...

ni kweli tulimpenda lakini ngoja tuamini kwamba mungu alimpenda zaidi, kama unakumbuka alikuwa best wa mystella wangu,alikuwa mpatanishi wa viuzushi vya hapa na pale vilivyokuwa vikijitokeza enzi zile tukiwa muccobs, alikuwa mdogo mkiumri lakini mwingi wa busara na ushauri ambao naamini umlinisaidia na kufanikiwa kupunguza masa...nga. unakumbuka egidio? mambo ya royal

Anonymous said...

kaka asanteni kwa ushirikiano, hii inanipa moyo kwamba masela 2ko 2gether katika msiba wa rafiki yangu mpendwa Prisca E. Nkanyila. niwagusie kitu kimoja, mpendwa wetu Prisca alifariki siku aliyozaliwa. Niko katika kipindi kigumu sana kwani Prisca alikua mtu wangu wa karibu sana na mshauri mzuri sana ktk maisha, najaribu kujiuliza mtu anapokufa tunasema kazi ya Mungu haina makosa, je Mungu anaua? tuwe pamoja masela wangu. asanteni.

chemshabongo said...

philipo naona umeamua kuji anony lakini tupo pamoja kaka! kazi ya mungu haina makosa, nilikuwa sijui kama birth day yake ndo imekuwa derth day yake

Simon Kitururu said...

Poleni sana !

chemshabongo said...

tunashukuru kaka kitururu kwa kutupa pole. tupo pamoja

Mija Shija Sayi said...

Poleni sana..

chemshabongo said...

damija fungate limeisha?
tunashukuru kwa kuwa pamoja, ahsante sana tumeshaanza kupowa

Christian Bwaya said...

Poleni sana kwa kutanguliwa na ndugu yenu. Tuko pamoja.

Anonymous said...

Polleni sana.

Mama Malaika